Translate

Jumapili, 8 Februari 2015

IJUE MITI MAARUFU TANZANIA
Ifuatayo ni baadhi ya miti maarufu Tanzania iwe ili pandwa au ilijiotea yenyewe.Baadhi ya miti imekuwa kivutio kutokana na historia na faida yake kwa jamii.Miti ni viumbe hai vinavyojumuisha uzito hai kama ilivyo kwa wanyama na uhai wake ni muhimu kwa dunia endelevu.Miti imechangia katika dhima mbalimbali iwe historia ,elimu,utamaduni,harakati na utalii.Miti ifuatayo ni maarufu kutokana na kuvutia watalii,wasomi na watu wadini na wa matambiko kutoka maeneo tofauti Tanzania na dunia kwa ujumla.
Mdegree Tree (FICUS)
Mti huu unapatikana katika chuo kikuu cha Dar es Salaam ni mti maarufu uliopandwa mwaka 1960 na raisi wa kwanza wa Tanzania Mwl J.‪#‎Nyerere‬.Mti huu ulioko mbele ya ukumbi wa Nkuruma hall unaopatia wanafunzi kivuli cha kusoma na kupata degree zao.Mahali pa mti huu ndipo harakati za maandamano na migomo ya wanafunzi huanzia.Mahali hapa pa mti huu pana mazingira mazuri ya kusomea pamoja na mtandao wa bure.

Mwembe waliokutana Dr David Livingstone na Stanley
Mwembe huu ulioko ‪#‎Ujiji‬ ‪#‎Kigoma‬ karibu na jumba la makumbusho la ‪#‎Dr‬Livingstone ndipo walipokutana wachunguzi karne ya 19.Mwembe huu uko chini ya idara ya Mali kale kama kumbukumbu ya historia ya bara.Mwembe huu mpaka leo umesimama na kuvutia watu mbalimbali duniani.

Afbeeldingen van Kigoma – vakantiefoto’s










Mbuyu wa kujificha Majangili (poachers hide)
Mti huu aina ya mbuyu(Adansonia digitata) unapatikana katika hifadhi ya taifa Tarangire.Hapo zamani mbuyu huu ulikuwa unatumika pango la kujificha majangili waliokuwa wanawinda wanyamapori ndani ya hifadhi.Mbuyu huu katikati unapango ambalo wanaweza kuingia takribani watu arobaini.Mbuyu huu unavutia watalii wanaotembelea hifadhi ya ‪#‎Tarangire‬ na ni mojawapo ya rasilimali ya utalii inayopatikana katika hifadhi ya Tarangire.2982398831_2b5a4ecb70_z.jpg

Mbuyu wa kanisa
Mti huu ni maarufu na muhimu kwa kanisa katoliki na historia yake ya kuenea kwa ukiristo Afrika Mashariki.Mbuyu huu unaopatikana katika mji mkongwe wa‪#‎Bagamoyo‬ ulipandwa mwaka 1860 na padri Anthony Horner kwa misheni ya Katoliki Bagamoyo.Mti huu jinsi unavyokuwa kwa Wakatoliki ndo jinsi imani ya Kanisa Katoliki linavyoenea Afrika Mashariki.Mti huu una baki ya mjororo uliokuwa unatumika kufunga punda wa muuguzi Madame de Chevalier mnamo mwaka 1895.






















Mvule wa Ajabu
Mvule wa Ajabu ni mti maarufu unaopatikana katika hifadhi ya msitu wa Rau‪#‎Moshi‬ inasemekana na Tanzania Tourist Board kwamba ndo mvule wenye umri mrefu ‪#‎Afrika‬.Mti huu wenye umri takribani miaka 194 umeweza kudumu umri huu katikati ya miti mingi muhimu ya mbao na sgughuli za binadamu kutokana na mila na desturi za wananchi wanaozunguka msitu huu.Historia inayo kwamba mti huu ulikuwa ukikatwa unatoa damu pamoja na shughuli za matambiko mti huu ukapona na kutimiza umri mrefu kati ya miti ya mivule Tanzania.Hii inaonyesha kwamba mila na desturi zetu za Mwafrika zilikuwa zinasaidia kuhifadhi mimea na wanyama toka kale.Mti huu ni rasilimali ya utalii katika ‪#‎Msitu‬ wa Hifadhi Rau.ndio maana Rau Rau eco and cultural tourism programme wanaendeleza mpango wao mahsusi wa utalii ikiwa kivutio kikubwa ni Mvule wa Ajabu.
Hii ni baadhi ya miti maarufu michache inayopatikana ‪#‎Tanzania‬ na ipo katika uhifadhi uwe wa Mali Asili au Mali Kale.Makala ni maalumu kwa kutambua michango miti katika historia,tamaduni na maisha yetu ya kila siku.
Imeandikwa na mkumbatia Mti Mckene Ngoroma ‪#‎TREEHUGGER‬

Jumamosi, 7 Februari 2015

Kutokomeza Umaskini wa Nishati Afrika

Kutokomeza Umasikini wa Nishati (KUNI) AFRIKA,
Ni mpango wa Eco Footprints Tz wa kujitolea na kuwezesha jamii kutokomeza umaskini wa nishati kupitia uelewa wa rasilimali endelevu pamoja na matumizi ya nishati jadidifu na kuhifadhi mazingira.
Mpango huu una mkakati wa kujitolea katika elimu, vitumizi na vichochezi vya nishati jadidifu  mfano  balbu jua,mkaa endelevu,majiko sanifu katika maeneo ambayo yameathirika na mabadiliko tabia nchi kutokana na ukataji miti ovyo na uharibifu wa misitu.Aidha baadhi ya maeneo hayo  yamepata elimu na uelewa kutoka mashirika mbali mbali kwa hiyo kujitolea katika maeneo haya ambayo yana umuhimu katika nchi kiekologia na haki za binadamu.

 Mfano Barafu iliyoko mlima Kilimanjaro inaendelea kuyeyuka na hii inachangiwa kimataifa na kitaifa kwa hiyo tukiwa kama wa ndani tunaona ni mchango wetu kushiriki “Kutokomeza Umaskini wa Nishati”KUNI ambayo inaleta mabadiliko tabia nchi na kuathiri haki za binadamu, jinsia pamoja na vyanzo vya vifo. Matumizi ya nishati hai ni endelevu kama itafuatiliwa na kuwa rasmi tutaendelea kushi na amani na asilia yetu.Tuna mpango wa kujitolea usanifu wa bidhaa rafiki mazingira pamoja na majiko sanifu,taa za solar na kutoa elimu ya kutengeneza vichochezi hai , kuongeza wigo mpana wa upatikanaji wa bidhaa  sokoni na kama chanzo cha mapato kwa kaya.

 Kutokana na kuvumbuliwa kwa mafuta na gesi Afrika mashariki hii inaleta kushiriki katika mchakato huu ili kuleta kufaidika kwa jamii na maendeleo endelevu na biashara ya  hewa ukaa inayotokana na kuvuna nishati ufu  na hii kwa upande mwingine inatakiwa kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. Biashara ya nishati enedelevu  inafaa kunufaisha jamii kupitia ujasiriamali wakuzalisha na kusambaza  bidhaa za nishati jua .

Kutokana na  ‘kufufua’ nishati ufu na kuhatarisha maisha ya viumbe hai nishati jadidifu ndio mkombozi wa baadae.Hivyo basi inchi za Afrika  yaani Kenya,Tanzania Uganda,Mozambique na Angola zitatokomezaje umasikini wa nishati  kupitia  mkongo off gird  na huku ikipunguza uzalishaji wa gesi joto kutokana na nishati ufu.

Mpango KUNI Afrika unafanya tathmini kwenye kila kaya inayojitolea vifaa tumizi nishati jadidifu hasa katika maeneo yaliyoathirika na ukataji na uharibifu wa misitu na umaskini wa nishati.Katika hili wanatumia ufuatiliaji wa upunguzaji hewa ukaa katika kaya kwa lugha ya kingereza indoor air pollution IAP.

”Biomass will remain the major source of energy for rural populations, coupled with niche renewables such as Solar PV, provided they are affordable, reliable and a proper payments system is established9”  Evance Kitui