Translate

Jumamosi, 11 Aprili 2015

Tanuru la Pipa la Chuma Cookswell Jiko ni Mkombozi  wa Misitu nchini Kenya

Uharibifu wa misitu na ukataji miti hovyo ni chanzo cha mabadiliko tabia nchi Duniani na uzalishaji wa hewa ukaa kama inavyoainishwa na MKUHUMI (REDDS) .Uzalishaji wa hewa ukaa kwenye anga  unachochewa na shughuli  za binadamu hasa uharibifu wa misitu (deforestation) na  kukata miti ovyo (forest degradation) kwa ajili ya kuanzisha masahamba na kutengeneza mkaa kama nishati ya majumbani.Utengenezaji huu wa mkaa kwa tanuru la udongo usio madhubuti umekuwa chanzo  cha kiwango kikubwa cha hewa ukaa inayopotea katika kitendo cha kukabonisha (carbonization) na kupata mkaa kidogo kulingana na kuni zilizoyotumika.

 Nchini Kenya kampuni ya bidhaa za kuhifadhi nishati Cookswell Jiko wameboresha na  kutengeneza tanuru la pipa la bati kwa kukabonisha matawi ya miti badala ya kukata miti ovyo na uharibifu wa misitu.Tanuru hili la pipa madhubuti  liloboreshwa na kusanifiwa Kenya na wasanii wa Kenya linakabonisha matawi ya miti,mapute ya nazi,magunzi ya mahindi na mianzi ili kupata mkaa rafiki mazingira (eco charcoal).Tanuru hili bora la kuhamisha ni mkombozi wa misitu na miti kwa sababu hauhitaji kukata miti kutengeneza mkaa kwa tanuru la udongo, bali kutumia matawi yaliyobanguliwa vizuri na kutengeneza mkaa mwenyewe (DIY).

Kwa kutumia tanuru hili la Cookswell Jiko utakuwa umeokoa misitu  na kupunguza hewa ukaa na kufanya Mkaa kuwa Nishati Jadidifu.Ukitaka kujua kuhusu bidhaa za kuhifadhi nishati kutoka Cookswell Jiko pamoja na majiko sanifu (efficiently cookstove),joko la kuikarisha (barbeque oven) na jiko la kuotea tembelea ukurasa wao wa face book na tovuti  yao.

Tanuru hili la pipa  linapatikana Tanzania kupitia Eco Footprints Tz.

Tanuri la pipa la chuma Cookswell Jiko  lililoboreshwa.  OKOA NISHATI: OKOA MISITU YETU



Imeandikwa na Mckene Ngoroma

Jumapili, 5 Aprili 2015

Historia ya Jiko banifu/Sanifu KCJ

Historia ya jiko sanifu barani Afrika inaanzia miaka ya 1970 na kuendelea mpaka miaka ya 1980.Tokea mwaka 1982 Shirika la Nishati na Mazingira Kenya KENGO lilifanya tafiti ikishirikiana na wataalamu wasomi mmojawapo ni Dr Maxwell Kinyanjui kufanya tafiti na kuendeleza matumizi ya jiko la ufinyanzi.Jiko hili lina chimbuko kutoka Thailand ambako lilianzia kutokana na jiko ‘ndoo’.Taasisi kama CARE,UNICEF na Bellerive zimefanya kazi kubwa kutoa mchango wa kifedha na kuwezesha kuendeleza jiko na namna ya kulitengeneza pamoja na mashirika ya misaada kama Marekani (USAID),Ujerumani (GTZ) na mashirika mengineyo. Mtaalamu,msanifu na msomi Dr Maxwell Miringu Kinyanjui kutoka Kenya  alifanikisha maendeleo ya jiko hili kuwa sanifu  na bora kwa matumizi ya nishati ndogo ya mkaa.Kutokana na tafiti,fafanuzi na biashsra ikafanya jiko sanifu  (ufinyanzi) kutambulika kama jiko la kupunguza matumizi  ya nishati ya kupikia mkaa Kenya.Kwa mara ya kwanza jiko kwenda sokoni lilikuwa linauzwa bei ghali kutokana na watumiaji wengi baadhi yao kuwa ni maskini wanaotumia jiko la mafiga matatu. Baada ya kufikiriwa kwa makini hitimisho lilifikiwa na wataalamu kwamba kutokana na jiko ni geni sokoni basi lisi wekewe ruzuku ili liende sokoni lishindane kama bidhaa nyingine na kuleta ushindani thabiti. Mwanzo jiko Sanifu (ufinyanzi) lilikuwa ghali,mauzo yalikuwa taratibu na ubora ulitofautiana kutokana na kuigwa utengenezaji na wasanifu wengine bila kufuata vigezo kuwa na majiko sanifu feki yasiyo na ubora kama ulio kusudiwa.Kuendelea  kuongezeka kwa watengenezaji na wauzaji wa majiko sanifu kukaongeza ushindani na hii ikaongeza uvumbuzi wa kutengeneza chaga za jiko kwa kutumia udongo ufinyanzi pamoja na simenti ili kupata chaga bora itakayo akisi joto na kukaa nalo muda mrefu.

Sehemu ya jiko

Jiko sanifu au jiko banifu lina  chaga ambayo ndio inayobeba mkaa wa moto na kuhifadhi  kutunza kwenye chaga amabayo imetengenezwa kwa udongo wa ufinyanzi ulio na uwezo wakuhifadhi  joto. Hivi sasa  chaga zinaboreshwa kwa  udongo ufinyanzi unachanganywa na simenti  kufanya chaga iwe ngumu na isiharibike mapema.Baadhi ya wasanifu na mafundi majiko wanaoiga jiko hili wamekuwa wakitengeneza chaga zisizo na ubora ulio kusudiwa. Baadhi ya watengenezaji wa majiko haya barani Afrika kama Cookswell Jiko Kenya na Tatedo Tanzania wanashauri chaga  bora ni zile zenye kudumu mda mrefu na uwezo wa kuhifadhi joto lisipotee kuonyesha uendelevu. Jiko hili Sanifu limechangia kukua ujasiriamali  kwa  watengenezaji wa majiko ya kawaida ya bati sasa hivi wanatengeneza  fremu ya jiko na chagga baada ya jiko hili kuwa maarufu katika kaya za Afrika Mashariki.

Kusambaa kuingia Tanzania

Jiko hili sanifu liliingia Tanzania miaka ya 1990 kutokea Kenya pale Shirika la Nishati Asili na Jadidifu Tanzania TATEDO kupata mafunzo kutoka kwa msanifu na muendelezaji  jiko hili barani Afrika Dr Maxwell Kinyanjui. Tatedo walikuwa wa kwanza  kueneza matumizi ya jiko hili na kuwezesha wajasiriamali wa nishati jadidifu ili kutumia jiko hili katika kaya za Tanzania.Mtaalamu wa Cookswell Jiko  Teddy Kinyanjui  anasema ili bidhaa ya jiko sanifu iweze kupenya sokoni inahitaji miaka 10 mpaka 20.Kwa hiyo kwa jiko sanifu (ufinyanzi) KCJ mpaka kufikia mwaka 2002 jiko sanifu lilikuwa limepenya soko la Tanzania na mpaka kufikia mwaka 2012 jiko hili lilikuwa linajulikana na maarufu kama jiko banifu,bora au sanifu. TATEDO wameendelea kupanua aina ya bidhaa hii ya jiko sanifu kwa kutengeneza aina mbalimabali za jiko hili kukidhi  mahitaji ya wateja mbali mbali kama Sazawa.

Faida ya Jiko sanifu

Yana punguza matumizi ya kichochezi nishati (mkaa) kwa asilimi sabini na moja 71%.
Hayachochei  uzalishaji wa moshi hewa ukaa (carbon).
Yana usalama wa joto na bati kutokana na joto kuhifadhiwa katika chaga bila kutorokea kwenye bati
Kumeongeza ajira kwa watengenezaji na ujasiriamali kwa viwanda vidogo vya kutengeneza chaga za ufinyanzi
Yanahifadhi nishati kwenye chaga
Yana dumu muda mrefu
Uzoefu unaonyesha yanapunguza gharama ya matumizi ya mkaa kwa asilimia hamsini 50%
Jiko Sanifu na Mkaa
Jiko hili linategemea mkaa unaotokana na mti ili kuchochea na kuhifadhi joto kwa matumizi ya kupikia.Kumekuwa na dhana potofu kwamba mkaa unatumika na maskini tu na hauna faida yoyote katika jamii au ni ‘nuksi’ katika uhifadhi wa misitu ya asili.Inashauriwa kupanda miti ilikuendelea kupata bidhaa ya mkaa inyotumika katika majiko banifu.Mkaa ni nishati jadidifu kama miti itakuwa inapandwa kwa ajili ya bidhaa mkaa.Pia kila mwananchi kupanda mti katika eneo lake analoishi ili kutengeneza mkaa wake mwenyewe (DIY) kwa kukabonisha  matawi ya miti,magunzi mapute ya nazi na kupata mkaa rafiki mazingira (eco charcoal).

 







Imeandikwa na Mckene Ngoroma kwa msaada wa vyanzo vya taarifa Teddy Kinyanjui  wa  COOKSWELL  JIKO KENYA na TATEDO Tanzania


Alhamisi, 2 Aprili 2015

Eco Footprints Tz ya shiriki kufanya Dar Es Salaam kuwa jiji safi mpaka kufikia 2020

Matembezi na Kuokota WALK &PICK SINZA-TANDALE-MAGOMENI 26 OCTOBA 2014


Tembea na okota ni mpango wa kufanya jiji la  Dar es salaam kuwa safi mpaka kufika  mwaka 2020 (clean Dar by 2020) mpango huu wa kutembea na kuokota taka unfanyika kila jumapili ya mwisho wa mwezi katika mitaa ya jiji la Dar es salaam. Mpango huu ni wakipekee katika aina za matembezi amabayo  nimekuwa nikijitokeza jiini Dar es Salaam. Katika kupinga utupaji taka ovyo wa jamii katika maeneo ya jumuiya na makaazi na kufikia malengo ya kuwa na jiji safi mpaka kufika mwaka 2020 (CLEAN DAR BY 2020). Tembea na okota au walk and pick ni matembezi yaliyoanzishwa na organization inayoitwa Voice Giving iliyoko Kinondoni . 

                               

  Matembezi haya ni ya aina yake  kwa sababu hauhitaji kupiga kelele au kubeba mabango kama ilivyozoeleka ila ni kutembea na kuokota taka taka pembezoni mwa barabara katika mitaa mbalimbali huku ukitoa elimu ya mazingira na kuhifadhi taka.Katika mataembezi haya  jamii  ina elimika ikikuona ukiokota taka kwakujiuliza  masawali mengi , wengine wakikufananisha na waokota  taka plastic kwa ajili ya mrudisho (recycling) wengine wakidhani umepewa pesa kuokota au wengine wakifikiria u wakala kutokana nakuvaa vifaa vya kujikinga. Watu wengine wanadhani  unaokota takataka mtaani kwao wakifikiri ni kisiasa na baadhi ya viongozi wa shinani na kata  wakitaka hata mtu anaejitolea kwa jamii  kama ilivyotokea pale mtaa wa Tandale uzuri eti mpaka uende kwenye ofisi ya kata kupata kibali. Baadhi wanakuliza unfanyia kazi kampuni gani na hii inajihidhirisha kwamba watu wako nyuma kujitolea katika jamii ya kufanya usafi wa mazingira hasa katika makazi yao eti mpaka wafanyiwe au waambiwe  Nipe Fagio. 


Kwa mpango huu uliobuniwa na vijana wa Voice Giving uko sambamba na shindano la WWF Earth Hour City Challeng  ambao umeingiza Dar es Salaam kushindania kuwa jiji safi na kupunguza hewa ukaa kwa kutumia nishati jadidifu na  kupanda miti. Ushirikishi wa jamii katika matatizo yao mfano kutoa elimu kwa wakazi na kuonyesha mfano kwa kufanya usafi wa mazingira na makaazi yetu pamoja na utupaji wa taka za platik sehemu zisizosahihi.Takataka zimekuwa zikizorotesha afya ya mazingira  hasa plastiki ambayo inachukua miaka 1000 kuoza  na kuleta athari mbali mbali katika viumbe hai nchi kavu na baharini.Tembezi  la tarehe 26 octoba  ni tembezi lililonipa changamoto ya kufikiria kwa upana  tatizo na suluhisho la kukabiliana na taka taka katika jiji la Dar es Salaam. Tembea na okota (walk and pick) ni moja ya matembezi ya harakati amabalo nimepata uelewa  na elimu ya kutosha   kama mjasirianali wa mazingira pamoja na kijamii kuhusu taka taka za Dar es salaam.Kuanzia Sinza kijiweni mpaka Shule ya Msingi Magomeni ni elimu niliyoipata katika uchafuzi wa mazingira na tabia za watu wa Dar es salaam katika muono wa taka taka.Kuchelewa kufika kwa halmashauri au watoa huduma ya taka kituoni na kukuta taka zimefurika huku ziki hatarisha afya za wakazi hasa kituo cha pili mtaa wa Tandale uzuri barabarani tulikuta lundo la takataka karibu namazingira wanayo cheza watoto.


Katika tembezi hili takataka nyingi mitaani ni plastic material pamoja na karatasi na maboksi ambayo ni rahisi kurudishwa.Ni baadhi ya maskini wa mijini wanajua habari ya mazingira na kutotupa taka ovyo mfano kuanzia sinza kijiweni mpaka darajani kuingia kata ya Tandale ina taka nyingi zikiwemo plastic za viroba.Mitaro ya maji machafu ndipo taka zilipo tulia ampapo wakazi wanachukulia urahisi huo huku wakisubiri mvua zinyeshe ziweze kusukumiwa  maeneo ya baharini.Taka nyingi ambazo ziko barabarani zinaweza kutokomezwa ikiwa abiria na wenye mabasi kupitia vyama vyao kama DAROBA wata shurutishwa kufuata sharia zilizowekwa tutaweza kutokomeza uchafuzi huu. Sisi wakaazi ndio wazalishaji wa taka taka hasa katika matumizi yetu ya kila siku kufanikisha mahitaji yetu.Hivyo basi hatuna budi kuhifadhi au kutupa taka sehemu sahihi  baada ya matumizi ya bidhaa zenye vifungashio vya mifuko ya plastiki au kukataa kabisa kufungiwa bidhaa na mifuko ya plastiki. Kila raia awe mhamasishaji wa kutotupa taka ovyo mfano kama mji wa Moshi kila raia anaogopa kutupa taka ovyo kutokana na sherika kali ya kutozwa faini shilingi elefu hamsini
  
hapa managing director wa Eco footprint tz akitembea na kuokota taka

Hapa Md wa Eco Footprints Tz akiongea na watoto kuhusu atahri za uchafu kituo cha pili Tandale
 kufika kituo cha kwanza cha taka taka mtaa wa tandale
Hapa MD wa Eco footprints Tz akitoa elimu ya mazingira