Translate

Jumatano, 23 Septemba 2015

Tanuru la Pipa la Chuma Cookswell Jiko ni Mkombozi  wa Misitu Afrika Mashariki

Uharibifu wa misitu na ukataji miti hovyo ni chanzo cha mabadiliko tabia nchi Duniani na uzalishaji wa hewa ukaa kama inavyoainishwa na MKUHUMI (REDDS) .Uzalishaji wa hewa ukaa kwenye anga  unachochewa na shughuli  za binadamu hasa uharibifu wa misitu (deforestation) na  kukata miti ovyo (forest degradation) kwa ajili ya kuanzisha masahamba na kutengeneza mkaa kama nishati ya kaya.

Utengenezaji  wa mkaa kwa tanuru la udongo usio madhubuti umekuwa chanzo  cha kiwango kikubwa cha hewa ukaa inayopotea katika kitendo cha kukabonisha (carbonization) na kupata mkaa kidogo kulingana na kuni zilizoyotumika. Nchini Kenya kampuni ya siku nyingi ya bidhaa za kuhifadhi nishati Cookswell Jiko wameboresha na  kutengeneza tanuru la pipa la bati kwa kukabonisha matawi ya miti badala ya kukata miti ovyo na uharibifu wa misitu.

Tanuru hili la pipa madhubuti  liloboreshwa na kusanifiwa Kenya na wasanii wa Kenya linakabonisha matawi ya miti,mapute ya nazi,magunzi ya mahindi na mianzi ili kupata mkaa rafiki mazingira (eco charcoal).Tanuru hili bora la kuhamisha ni mkombozi wa misitu na miti kwa sababu hauhitaji kukata miti kutengeneza mkaa kwa tanuru la udongo, bali kutumia matawi yaliyopogolewa vizuri na kutengeneza mkaa mwenyewe (DIY).

Kwa kutumia tanuru hili la Cookswell Jiko utakuwa umeokoa misitu  na kupunguza hewa ukaa na kufanya Mkaa kuwa Nishati Jadidifu.Ukitaka kujua kuhusu bidhaa za kuhifadhi nishati kutoka Cookswell Jiko pamoja na majiko sanifu (efficiently cookstove),joko la kuikarisha (barbeque oven) na jiko la kuotea tembelea ukurasa wao wa face book @Cookswell saving jiko.
Tanuru hili la pipa  linapatikana pia Tanzania kwa wasambazaji wa bidhaa rafiki mazingira na nishati jadidifu Eco Footprints Tz na mradi wa kutokomeza umaskini wa nishati KUNI AFRIKA.





                                                         OKOA NISHATI: OKOA MISITU YETU


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni