Translate

Alhamisi, 2 Aprili 2015

Eco Footprints Tz ya shiriki kufanya Dar Es Salaam kuwa jiji safi mpaka kufikia 2020

Matembezi na Kuokota WALK &PICK SINZA-TANDALE-MAGOMENI 26 OCTOBA 2014


Tembea na okota ni mpango wa kufanya jiji la  Dar es salaam kuwa safi mpaka kufika  mwaka 2020 (clean Dar by 2020) mpango huu wa kutembea na kuokota taka unfanyika kila jumapili ya mwisho wa mwezi katika mitaa ya jiji la Dar es salaam. Mpango huu ni wakipekee katika aina za matembezi amabayo  nimekuwa nikijitokeza jiini Dar es Salaam. Katika kupinga utupaji taka ovyo wa jamii katika maeneo ya jumuiya na makaazi na kufikia malengo ya kuwa na jiji safi mpaka kufika mwaka 2020 (CLEAN DAR BY 2020). Tembea na okota au walk and pick ni matembezi yaliyoanzishwa na organization inayoitwa Voice Giving iliyoko Kinondoni . 

                               

  Matembezi haya ni ya aina yake  kwa sababu hauhitaji kupiga kelele au kubeba mabango kama ilivyozoeleka ila ni kutembea na kuokota taka taka pembezoni mwa barabara katika mitaa mbalimbali huku ukitoa elimu ya mazingira na kuhifadhi taka.Katika mataembezi haya  jamii  ina elimika ikikuona ukiokota taka kwakujiuliza  masawali mengi , wengine wakikufananisha na waokota  taka plastic kwa ajili ya mrudisho (recycling) wengine wakidhani umepewa pesa kuokota au wengine wakifikiria u wakala kutokana nakuvaa vifaa vya kujikinga. Watu wengine wanadhani  unaokota takataka mtaani kwao wakifikiri ni kisiasa na baadhi ya viongozi wa shinani na kata  wakitaka hata mtu anaejitolea kwa jamii  kama ilivyotokea pale mtaa wa Tandale uzuri eti mpaka uende kwenye ofisi ya kata kupata kibali. Baadhi wanakuliza unfanyia kazi kampuni gani na hii inajihidhirisha kwamba watu wako nyuma kujitolea katika jamii ya kufanya usafi wa mazingira hasa katika makazi yao eti mpaka wafanyiwe au waambiwe  Nipe Fagio. 


Kwa mpango huu uliobuniwa na vijana wa Voice Giving uko sambamba na shindano la WWF Earth Hour City Challeng  ambao umeingiza Dar es Salaam kushindania kuwa jiji safi na kupunguza hewa ukaa kwa kutumia nishati jadidifu na  kupanda miti. Ushirikishi wa jamii katika matatizo yao mfano kutoa elimu kwa wakazi na kuonyesha mfano kwa kufanya usafi wa mazingira na makaazi yetu pamoja na utupaji wa taka za platik sehemu zisizosahihi.Takataka zimekuwa zikizorotesha afya ya mazingira  hasa plastiki ambayo inachukua miaka 1000 kuoza  na kuleta athari mbali mbali katika viumbe hai nchi kavu na baharini.Tembezi  la tarehe 26 octoba  ni tembezi lililonipa changamoto ya kufikiria kwa upana  tatizo na suluhisho la kukabiliana na taka taka katika jiji la Dar es Salaam. Tembea na okota (walk and pick) ni moja ya matembezi ya harakati amabalo nimepata uelewa  na elimu ya kutosha   kama mjasirianali wa mazingira pamoja na kijamii kuhusu taka taka za Dar es salaam.Kuanzia Sinza kijiweni mpaka Shule ya Msingi Magomeni ni elimu niliyoipata katika uchafuzi wa mazingira na tabia za watu wa Dar es salaam katika muono wa taka taka.Kuchelewa kufika kwa halmashauri au watoa huduma ya taka kituoni na kukuta taka zimefurika huku ziki hatarisha afya za wakazi hasa kituo cha pili mtaa wa Tandale uzuri barabarani tulikuta lundo la takataka karibu namazingira wanayo cheza watoto.


Katika tembezi hili takataka nyingi mitaani ni plastic material pamoja na karatasi na maboksi ambayo ni rahisi kurudishwa.Ni baadhi ya maskini wa mijini wanajua habari ya mazingira na kutotupa taka ovyo mfano kuanzia sinza kijiweni mpaka darajani kuingia kata ya Tandale ina taka nyingi zikiwemo plastic za viroba.Mitaro ya maji machafu ndipo taka zilipo tulia ampapo wakazi wanachukulia urahisi huo huku wakisubiri mvua zinyeshe ziweze kusukumiwa  maeneo ya baharini.Taka nyingi ambazo ziko barabarani zinaweza kutokomezwa ikiwa abiria na wenye mabasi kupitia vyama vyao kama DAROBA wata shurutishwa kufuata sharia zilizowekwa tutaweza kutokomeza uchafuzi huu. Sisi wakaazi ndio wazalishaji wa taka taka hasa katika matumizi yetu ya kila siku kufanikisha mahitaji yetu.Hivyo basi hatuna budi kuhifadhi au kutupa taka sehemu sahihi  baada ya matumizi ya bidhaa zenye vifungashio vya mifuko ya plastiki au kukataa kabisa kufungiwa bidhaa na mifuko ya plastiki. Kila raia awe mhamasishaji wa kutotupa taka ovyo mfano kama mji wa Moshi kila raia anaogopa kutupa taka ovyo kutokana na sherika kali ya kutozwa faini shilingi elefu hamsini
  
hapa managing director wa Eco footprint tz akitembea na kuokota taka

Hapa Md wa Eco Footprints Tz akiongea na watoto kuhusu atahri za uchafu kituo cha pili Tandale
 kufika kituo cha kwanza cha taka taka mtaa wa tandale
Hapa MD wa Eco footprints Tz akitoa elimu ya mazingira 










Maoni 3 :

  1. Shukrani Suavity products tunaleta mabadiliko kwenye mitaa yetu, let keep #zerowaste

    JibuFuta
  2. Naamini kwa pamoja tuta enzi asili yetu na mm ninatengeneze chaga za majiko nomba tuwasiliane kama mtakua na uhitaji 0654343308

    JibuFuta